Bomu lililotegwa ndani ya gari lilipiga mgahawa uliokuwa umejaa mashabiki wa soka wakitazama fainali ya Euro 2024 kati ya Uhispania na Uingereza mjini Mogadishu Jumapili usiku.

Idadi ya watu waliofariki kutokana na mlipuko katika mgahawa mmoja katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu imepanda hadi tisa, vyanzo vya usalama vililiambia shirika la habari la AFP siku ya Jumatatu, baada ya gari lililokuwa limetegwa bomu kushambulia uwanja huo uliokuwa umejaa mashabiki wa soka wakitazama fainali ya Euro 2024.

“Raia tisa waliuawa na wengine 20 kujeruhiwa katika mlipuko huo,” Mohamed Yusuf, afisa kutoka wakala wa usalama wa taifa alisema, na kuongeza idadi rasmi ya watano iliyotolewa na mamlaka Jumapili jioni.

“Kulikuwa na watu wengi ndani ya mgahawa huo, wengi wao wakiwa ni vijana waliokuwa wakitazama mechi hiyo ya mpira wa miguu… lakini shukrani kwa Mungu, wengi wao walitoka salama baada ya kutumia ngazi kupanda juu na kuruka ukuta wa pembeni ya nyuma,” alisema.

By Jimmy

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *